Saturday, September 6, 2025

GHARAMA YA USHINDI

 GHARAMA YA USHINDI

1. Utangulizi

2. Gharama ya ushindi

3. Kudumu kuwa mshindi


Sehemu ya kwanza. Utangulizi 

Kila jambo unalo ona limekwisha fanyika, linafanyika sasa au imepangwa kufanyika baada ya wakati fulani, katika mpango wake Kuna kipengele cha gharama.

Gharama ya jambo inaweza kwa sehemu kubwa kuamua thamani ya Hilo jambo hilo ikishirikiana na matokeo yake. 

Tutajikita zaidi kuangalia gharama ya ushindi katika mambo yamuhusuyo mwanadamu hapa duniani. (Maisha) 

Kwa sababu maisha ni jambo pana lenye tafsiri nyingi nitajitahidi kueleza bila kutumia misamiati migumu na Kwa lugha inayoeleweka. Twende pamoja. . .

Gharama ni aidha muda, nguvu, fedha, mali, maumivu, ufahamu/ujuzi, aina ya maisha, aina ya kazi na mambo yanayofanana na hayo yanayofanyika ili kufanikisha jambo lililokusudiwa Kwa muda mfupi au muda mrefu. 

Mfano wapo watu waliolazimika kuishi maisha ya chini ili wahakikishe wanakamilisha ujenzi, wapo waliolazimika kuongeza ujuzi au kisomo ili wapate aina fulani ya kazi.

Zote hizo ni gharama za ushindi wa Yale waliyo yakusudia. 

Wakati unapanga kufanya jambo au kama hukupanga na umejikuta upo ndani ya jambo, jiulize swali la hili, "ni zipi gharama za jambo hili kufanikiwa?"

Unapozifahamu gharama ni rahisi kuishi kulingana na matakwa ya mafanikio ya jambo lako. 

Wakati mwingine kuzifahamu kunaweza kuhusishwa na woga au hofu juu ya jambo husika, lakini Bado ni muhimu sana kufahamu gharama za kushinda. 

Unapo ona biashara ya mtu inaenda vizuri ujue kabisa kuna gharama ya kusababisha iende hivyo. Unapo ona ndoa ya mtu inaenda vizuri ujue Kuna gharama! Unapo ona maisha ya mtu kidogo yanaenda sawa ujue kuna gharama. 

Kwa lugha nyingine rahisi ki tekinolojia, Kila mara tunachaji vifaa vyetu vya mawasiliano ili kuhakikisha tunaweza aidha kupatikana au kuwapata tunaowatafuta. 

Vivyohivyo tunaweka salio kwenye vifaa hivyo ili tuweze kuwa hewani. Maana yake tumeingia gharama ya kuhakikisha yaliokusudiwa yanafanikiwa. 

Zoezi

1. Andika mambo matatu unayojishughulisha nayo katika maisha yako.

2. Ainisha gharama ya mambo hayo. 


Sehemu ya pili. Gharama ya ushindi 

Kwa kiasi sasa tumeshatambua tunacho kumbushana. 

Zifuatazo ni gharama ambazo zinahusika katika kufanikisha ushindi wa mtu au watu katika jambo lililokusudiwa. 

1. Uhusiano na Mungu. 

Huu ni msingi mkuu wa ushindi. Msingi huu unaweza kujitosheleza kabisa kwa ajili ya ushindi. 

Mahusiano na Mungu yanapimwa kuanzia kiwango cha matumizi yako ya muda. 

 Uliongea na Mungu lini mara ya mwisho wewe peke yako, Kwa sababu yako mwenyewe, au kuhusu biashara yako, au kuhusu ndoa yako, kuhusu mradi wenu, taasisi au jamii yenu..? 

Umetenga muda kwa ajili ya mambo yako yote lakini je Mungu amepata nafasi katika muda wako wa siku? 

Sisemi kwamba Kila siku uende kukusanyika katika ibada, ila nasema kwamba Kila siku unaweza kuwa na muda mfupi wa kuzungumza na Mungu wako. 

Amebarikiwa mtu yule amtegemeaye Bwana, atakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya maji.. Mtu anayeboresha mahusiano yake na Mungu ameunganishwa na asili ya mafanikio yake moja kwa moja. Haishiwi, hafilisiki, harusi nyuma kwasababu ameunganishwa na vyanzo vya baraka, ameunganishwa na vyanzo vya ufahamu bora Kwa ajili ya mafanikio yake. ( Mimi ni Mungu nikufundishaye ili upate faida). Taasisi yenye mahusiano na Mungu kadhalika haiwezi kurudi nyuma. 

Kuweka mahusiano mazuri na Mungu ni sawa na kuweka mahusiano na mafanikio yako. 

Wengi hujiuliza nitaanzia wapi au mbona Nina mahusiano mazuri na Mungu. 

Kwa mtu binafsi unaweza kuanza na hii. 

     Kila asubuhi unapojiandaa tenga dakika Tano za kumweleza Mungu kuhusu ratiba yako ya siku husika kisha mwombe akutangulie. Inapofika mchana, angalia dakika tano mueleze kuhusu siku yako jinsi inavyoenda na kumshukuru. Dakika tano tu sio nyingi. Inapofika jioni unaporudi mahali unapojipunzisha, kabla ya mambo mengi, mda mfupi Tena dakika tano mshukuru Mungu kwa siku na tambua aliyokusaidia ukiweza kuandika mahali ni vizuri zaidi. Jikabidhi tena mbele zake kwa muda huo. 

Kwa taasisi kabla ya mambo kuanza, katikati ya siku na baada ya kumalizia siku ifanyike hivyo. Kinachojengeka hapa ni ule utamaduni wa mawasiliano na Mungu. Na ndani yake utamaduni wa ratiba na mpangilio wa siku. Baada ya hapo utamaduni wa kupata mtazamo wa wiki, mwezi hadi Mwaka kuhusu yale uliyokusudia.

Uhusiano wako na Mungu ujikite kumfahamu. Aliwapenda zaidi watu wa namna gani au anafurahishwa na watu gani. Ni kina nani anao wafanikisha.?

Utaona Mungu anawapenda wale wanaompenda, anatokea Kwa wale wanao mtafuta, anawafanikisha wale wanaojibidiisha huku wakintegemea, anawasamehe wale eanaosamehe wengine, anafanya kazi na wale wenye kupenda kumfahamu, anawaongezea baraka wale wenye ufahamu wa kuzimudu au wenye utayari wa kuongeza Maarifa ya kuzimudu baraka hizo. 

Hivyo Kila anayeboresha mahusiano yake na Mungu anaweza kuwa mshindi katika mambo yamuhusuyo. 

Zoezi
Andika mambo kumi uliyofanya siku ya Leo.
Katika mambo hayo, kuna lililojikita kuboresha uhusiano wako na Mungu moja kwa moja? 

2. Uhusiano na watu

Kwasababu huwezi kumpenda Mungu usiye mwona wakati jirani unayemwona unamchukia, na kwasababu Mungu huwatumia watu ili kufanikisha mtu basi ufahamu ukiwa na huduma yeyote unayoitoa kwa jamii au ukihutaji huduma yeyote utahitaji watu. 

Uhusiano wako na watu utakuongezea sifa njema au sifa mbaya.  

Ili uweze kuwa mshindi ni muhimu kujifunza tabia za watu na namna ya kuhusiana nao, kuzifahamu tamaduni zao, maisha yao na mambo wanayoyataka ili uweze kujua ni mpaka gani usivuke na ni wapi hadi wapi ufike bila kuathiri mahusiano Yako na Mungu

Husiana na watu sana kwa kila namna nzuri lakini hakikisha mahusiano yako na Mungu hayaharibiki. 

Sehemu ya tatu . Kudumu kuwa mshindi

Ni rahisi tu, kuendelea kufanya yake yaliyokugikisha katika ushindi ni njia Bora ya kutunza ushindi wako. Bila kusahau kuongeza ufahamu kila mara juu ya namna ya kuendelea kudumu hapo.

Mambo yanayosababisha ushindi kuondoka katika maisha ya mtu, taasisi,familia au jamii.

1. Majivuno. Hali ya kuona kwamba ni kwasababu ya nguvu na juhudi zako au zenu 

Maneno ya kejeli kwa walio chini au ambao hawajafikia hatua hiyo. 

2. Tamaa. Tamaa ya mali au tamaa ya mwili. Kuipa nafasi tamaa kunasababisha mahusiano yaako na Mungu yanaharibika na hivyo mahusiano yako na ushindi wako, huondoa heshima yako kwa jamii yako na hivyo kubandua kidogo kidogo mafanikio yako kama ukoma. 

3. Marafiki/ washauri wabaya. 

Ukikosa ushauri mzuri au watu uliowafungulia moyo wako wakiwa waovu basi jiandae kuelekea njia hiyo hiyo. 

Jitahidi kuepuka marafiki wasio faa kwa gharama zote. 

Usiifiche Imani yako wala usimfiche Mungu wako mana yeye ndiye chanzo cha mafanikio yako. 

Hayo na yanayofanana na hayo yakifanikiwa kuharibu mahusiano yako na Mungu basi ufahamu umepoteza ushindi wako tayari hata kama Bado unaonekana kushinda. 

Mungu akubariki kwa wakati wa kujifunza. 

@David Edwin +255 754 914 944

Tuesday, May 6, 2025

WATU WANGU WAJIBU WANGU. MY PEOPLE MY RESPONSIBILITY

 ✓ WATU WANGU WAJIBU WANGU

✓My people my responsibility

*NI MUHIMU KUFAHAMU KWAMBA UNATAWAJIBIKA KWA WATU WAKO KATIKA MAMBO YOTE. YAANI YAKIWA YA FURAHA AU YA HUZUNI LAZIMA KUNA NAMNA YATAKUHUSU

It's important to understand that you'll be responsible for your people in everything. If they mourn or they celebrate in one way or another you'll be involved. 

*IKIWA UTASIMAMA KWA UAMINIFU NA KATIKA MAJUKUMU YAKO YOTE BILA KUONA HAYA BASI WATU WAKO WATAKUA SALAMA WAKIISIKIA SAUTI YA MUNGU KUPITIA KWAKO.

If you'll faithfully stand and in all your responsibility may be (as a leader/father), your people will be safe if they'll listen to the voice of God as He speaks through you.

*INAWEZA TOKEA BAADHI YAO WASIKUSIKILIZE, HAO WATAPATA HASARA KUBWA! SIO YA MALI TU HUENDA HATA MAISHA YAO. 

It might happen that they don't listen to you . They'll have great loss not only of material things or wealth but even their lives. 

*KAMA JAMBO BAYA LITATOKEA MAHALI NA MCHA MUNGU YUPO NA IKAWA KIMYA AU BILA TAARIFA BASI KUNA MAMBO HAYAKUKAA SAWA. 

If a bad thing will happen at a certain place and a righteous man/woman  is there without any information, something will be  probably wrong somewhere. 


* KAMA UKISIMAMA KATIKA NAFASI YAKO KWA UAMINIFU, BASI UFAHAMU YA KWAMBA UTALETA USALAMA SIO WAKO TU HATA WA WATU WAKO. (WALE WATAKAO SIKIA NA KUKUBALI KUTII)


If you faithfully stand at your position, you and your people will be safe but only if they'll listen and accept the truth. 


*MWANZO 19:12

*BASI WALE WATU WAKAMWAMBIA LUTU, JE! UNAYE MTU HAPA ZAIDI? MKWE, WANAO, NA BINTI ZAKO, NA WO WOTE ULIO NAO KATIKA MJI, UWATOE KATIKA MAHALI HAPA;


Genesis 19:12

And the men said unto Lot, Hast thou here any besides? son in law, and thy sons, and thy daughters, and whatsoever thou hast in the city, bring them out of this place:

ILI YATOKEE SHUGHULIKIA USIKU. DEALING WITH THE NIGHT TO BRING OUT RESULTS

ILI YATOKEE, SHUGHULIKIA USIKU


Dealing with the night to bring out results. 


•MAJIRA YALE AMBAYO ADUI ANAFIKIRI UMELALA HAPO NDIPO UNA AMKA NA KUIDAI HATMA YAKO MIKONONI MWA ADUI. 

When the enemy thinks you are asleep, it's when you rise and claim your destiny from the hands of your enemy. 

•KAMA MTOTO WA MUNGU UNAONA KUNA JARIBU LIMEKUKARIBIA USIHANGAIKE HUKU NA KULE. AU KULALAMIKA AU KULAUMU HAPANA!

As a child of God, whenever you find your self in temptation, don't begin to lament or deal with it like how others do.. No!

•AMKA USIKU IANDIKE HIYO HALI, HILO JARIBU, HUO MSIBA, HICHO KILIO, HAKIKISHA UNAKIANDIKA KWA MAPANA YAKE. 

Get up in the night, write that issue down, that pain, that cry and any sort of challenge you are through. Analyze it properly 

•USIZUNGUMZE NA WATU WENGI ANZA KUFANYIA KAZI. INGIA KWENYE MAOMBI.

Don't try to share it with many people.. just pray!! 

•KUNA BAADHI YA WATU UNAWEZA KUWAELEZA KUMBE WANAHUSIKA NA HALI UNAYOIPITIA.

Because some of the people you share with might be responsible with what you are going through.

•USIPO AMKA ADUI WALA HANA HURUMA. 

If you won't get up the enemy is merciless. 

•USIPO AMUA ADUI ATAENDELEA KUZOEA KUKUCHEKA.

If you don't decide the enemy will continue to mock you. 

NEHEMIA 2:12

KISHA NIKAONDOKA USIKU, MIMI NA WATU WACHACHE PAMOJA NAMI; WALA SIKUMWAMBIA MTU NENO HILI ALILOLITIA MUNGU WANGU MOYONI MWANGU, NILITENDE KWA AJILI YA YERUSALEMU; 


Nehemiah 2:12

And I arose in the night, I and some few men with me; neither told I any man what my God had put in my heart to do at Jerusalem: 

Thursday, January 2, 2025

MAMBO YA MUHIMU 2025

Namshukuru Mungu Kwa kutuvusha tena Kwa ushindi mwaka huu. 

Utangulizi

Wakati najiandaa na kumuomba Mungu juu ya Yale ninayotamani kuyafanya Mwaka 2025, Roho mtakatifu alinielekeza pia kuomba ili nifahamu Mungu amekusudia jambo gani kwangu Mwaka huu.

#. Kwanza kabisa, ni vizuri kuwa na mipango lakini ni muhimu kufahamu kwamba Mungu anayo mipango yake pia kulingana na majira ya maisha Yako.

Naona una malengo yako lakini Je! unayafahamu malengo ya Mungu juu Yako?

Utayafahamuje? nenda kwenye kikao barazani pa Bwana. Tenga muda mchache wa muhimu wa kuyaombea hayo uliyopanga na atakuambia lipo litafanyika na lipi lianze Tena Kwa namna gani lianze. Kina nani ushirikiane nao n.k na kama asipo kupambia Kwa sauti ataruhusu ufahamu uhalisia wa watu unaoshirikiana nao ili aweke umakini ndani yako wa namna ya kufanya nao kazi. 

Anaweza pia kuruhusu usome kitabu muhimu au uhudhurie semina itakayo fungua mawazo na ufahamu wako juu ya Hilo jambo.

Mambo Muhimu 

1. Mahusiano na Mungu. 

Unafanya kazi kubwa sana kuzitafuta nguvu za Mungu kuliko kazi ya kuzilinda

 Hii ni hatari kwako kwasababu ni sawa na mtu anayetafuta Mali Kwa gharama kubwa alafu anazitunza kwenye nyumba isiyo fungwa milango. Utapoteza muda mwingi, bila matokeo unayoyataka. Kuna mambo yatahitaji mahusiano yako na Mungu kuwa mazuri ili yatokee bila kutumia nguvu kubwa. 

Yakobo 4:8 (Kumkaribia Mungu naye kutukaribia)  

Kama utalinda kile unachopokea kwenye ibada ya katikati ya wiki au ibada ya jumapili basi kufunga na kuomba kitakua ni Kwa ajili ya Yale mengine yasiyowezekana isipokuwa Kwa kufunga na kuomba. 

Ameniambia hakuna maana ya kukesha kumwomba Mungu alafu huwezi kukesha kulinda ulimi wako, kulinda moyo wako, kulinda mawazo Yako, macho Yako n.k 

Lazima uelewe kwamba nguvu za Mungu unazopokea ni za thamani sana usizipoteze kihivi hivi tuu. 

2. Matumizi ya muda 

Muda wako wa thamani unautumiaje?

Mfano mrahisi, simu yako vs bibilia Yako. Najua simu ina bibilia pia. Na simu ina vitabu. Ila pia simu ina TikTok, fb, insta, na hata huko unaweza pata mambo ya kuongeza thamani.  Suala kubwa ni kuwa makini na matumizi ya muda wako na juu ya kufahamu je hili ninalolifanya hapa linaniongezea thamani au linaniongezea changamoto?

Kama Mwaka huu utatumia muda mwingi kwenye mambo yasiyo kuongezea thamani basi jiandae kupunguza kiwango cha ufaulu wa mipango yako.


Badala ya kujua nani amefanya Nini, unaweza kujikita kujifunza mambo mapya au kuongeza ujuzi kwenye Yale unayoyafanya kupitia hiyo hiyo simu yako. 

Sina ugomvi na simu ila, nakukumbusha uwe (specific) na kile  unachokifanya kwenye simu yako. 

Kina matokeo gani kwako? Ukikuta matokeo hayakufai achana nacho. 

Nitaendelea. 


3. Mahusiano na Watu. 

Ni wazi kwamba watu ndio huinua watu wengine, lakini pia Watu ndio wanaoweza kukushusha. Napenda kurejea baadhi ya maneno ya kiongozi wetu mkuu katika nchi Mhe. Samia Suluhu Hassan, "Watu ni mashahidi wa Mungu".  

Mwaka huu jitahidi sana kuwa na mahusiano rafiki kwa ajili ya hatma yako. Utafanikiwaje? 

Kwanza yale unayopenda kufanyiwa, wafanyie wengine. Usipoteze muda na watu ambao hawaongezi thamani katika maisha yako. Sijasema uwadharau, hapana!!  Sijasema uwapuuzie, hapana ila linda sana matokeo wanayoweza kuya leta kwako mnapokuwa pamoja nao. 

Tafuta ukaribu na watu wenye ndogo kubwa, watu wenye maono makubwa, bila kuwadharau hawa wadogo. 

Mwaka huu mtu asiye na matokeo asikushauri! Unaweza kusikiliza hekima zake ila usiziweke moyoni mana mara nyingi kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake. 

Katika kuhusiana na watu, tengeneza thamani yako, watu sahihi watavutika kwako. Ni vizuri kutumia nguvu kuwatafuta watu wapya lakini ni vizuri zaidi kuboresha vile ulivyo mana watu wa thamani watakutafuta tu!. 

Unaboreshaje? Unavaaje kama mtu mwenye safari ya ukuu au kama watu wa kawaida? Unazungumzaje? Unashiriki kwa namna gani kwenye mambo ya wengine, vipi matumizi yako ya fedha(tuytaizungumzia zaidi hii pia), ushiriki wako kwenye jamii iliyopo karibu nawewe je? 

Mtu akikusikiliza Kwa dakika kumi anaweza kufahamu ni mtu wa namna gani. Kichwani kwako umeweka vitu gani? Njia ya mwanzo ya kujiongezea thamani ni kuongeza ufahamu wako. 

Tafuta eneo moja ambalo unalipenda au unalifanyia kazi alafu ujikite kuongeza ufahamu katika hilo eneo, japo sio lazima liwe eneo lako la kiutaalamu.  

4. Nidhamu ya fedha.  

Unapenda kutumia kiwango ambacho hakiendani na kiasi unachoingiza. 

Nidhamu ya fedha inaendana na ufahamu sahihi wa elimu ya umiliki wa fedha ambayo mara nyingi haifundishwi shuleni. 

Unaweza kujifunza Kwa watu waliofanikiwa au kupitia vitabu vingi ambavyo vimeeleza juu ya nidhamu ya fedha au namna ya kuimiliki. 

Kwa kifupi tu mwaka huu kama hujaorodhesha mipango yako bado, unahutaji kukaa na kufanya hiyo kazi. Na mpango wa kwanza uwe kuweka akiba ya angalau matumizi yako ya miezi mitatu. 

Maana yake hapo uweke kiasi Cha pesa ambacho utakua na uhakika wa kuendelea kuishi Kwa miezi mitatu mfululizo hata usipo pata ingizo lolote jipya la kipato Kwa muda huo. 

Hii inakupeleka moja kwa moja kwenye bajeti. Unaijua bajeti yako ya mwezi? Hii inakulazimisha utafute kufahamu ratiba ya matumizi, chakula, safari n.k 

Tabia ya kutumia kwasababu vipo, au kupooza moyo kama wanavyodai wengine imesababisha watu wakachukulia poa fursa walizokutana nazo ambazo zingebadilisha maisha yao. 

Hii ndiyo sababu unaweza kumkuta mtu asiye na kipato maalum akifanya maendeleo wakati mwenye kazi na kipato maalum akiwa hajafanya chochote. 

Mfano mdogo

Ukinunua simu ya milioni moja wakati unauwezo wa kununua ya milioni tatu, huo ni ufahamu wa kiuchumi. 

Lakini..

Ukinunua simu ya milioni moja wakati uwezo wako ni wa kununua ya milioni moja, hilo ni kosa la kiuchumi. 

Haya sio maneno mageni mjini, labda Kwa mgeni mjini. Mwaka huu tujifunze sana namna ya kumudu fursa zinazopita mikononi mwetu, ili tusije kufika mwisho na majuto ya kutokufanya vizuri. 

Nitaendelea. . 







  

Tuesday, March 28, 2023

THE GOOD WINE 🍷

THE GOOD WINE  🍷
John 2:10
And saith unto him, Every man at the beginning doth set forth good wine; and when men have well drunk, then that which is worse: but thou hast kept the good wine until now.

Shalom brethren!
I wanna speak a little bit about
 "THE GOOD WINE" 
 As from our reference.. There's a norm that people are used to. There's a traditional practice of doing or handling things. 
Traditionally there are double standards. If not with economic aspect then age, if not age, then popularity, position/authority, gender, tribal, region/origin and any other phenomena that can be used to group people.

Have you ever walked to a parking with reservations? What about an event with seats reserved for so and so...
So let's go now..
1. At the beginning.•°••°•
 External appearance of something,. Before understanding the innermost characters of something/someone. 
Before getting into it
Before you start that ministry 
Before you start that behavior/lifestyle
Before you get into that crew of gamblers
Before you begin to pursue her/him
Before you start going for your dreams/purpose 
Every man at the beginning doth set good wine..


2. And when men have well drunk..° °•°•°•°
After you get what you thought you saw, or needed. After you've achieved getting her heart/his affection. 
After you've married her/him
After you've got into something you thought it was pleasant/ that would give you joy/peace/ pleasure 
When you've now come to a place of achievement
When you've now successfully managed your credits
When you've got all you wanted/prayed for.

3. Then that which is worse is brought°•°•°°••°•••
When the ups and downs arise a real character mist show up
When temptations rise some people astray from from the will of God.
Some forget or neglect the standards after achieving their goals. 
They don't offer the best service again.
No longer available in church service.
Not humble as in the beginning.. they've got what they wanted.
Not hardworking anymore
They are not ready to serve again, love again or cherish their spouses. They've arrived where they wanted to.
Now you're with the real person
With the original somebody
No more camouflages 
You can only see the true colors.
 
4. But thou hast kept the good wine until now. 🍷
What does keeping good wine until now mean? 

Maintaining the standards of..
Quality
Holiness 
Righteousness
Hard working
Love
Concern
Care
Humbleness
Wisdom
Humility
The outside you being the same as the inside you
Character etc...

Generally can we just conclude it as Taste/ Ever-tasty

Qn. How can this be achieved?
Here's a clear simple way to make it.
Jesus did a miracle He turned water into fine/good/standard wine.
What ever you need/you've been through in your life, just repent and pray this short powerful prayers with me. 
   Jesus, I believe that you are the son of God, and that you gave your life on the cross that I may have everlasting life. 
Please forgive all my sins and make me whole again.
In Jesus name I pray. Amen

Dear brethren. What you've done is now like filling  your water pots with water. Jesus is going to turn that water into fine-good wine. 

Be blessed as you live a life of testimonies in Jesus name. 
EVER-TASTY

Saturday, March 25, 2023

THE HEART OF ENQUIRY

Greetings in the name of our Lord and savior Jesus Christ.
Today I want to share a word of God with the tittle, "THE HEART OF ENQUIRY" 
May we pray Before we begin. 
Father in the mighty name of Jesus. We thank you for giving us this opportunity to share your word. Your word is life Dear God. May it reform our spirits to your will,  rekindle the fire in us, bring hope and revive the inner man. In the name of the father, the son and the holy spirit we pray. Amen.

SHALOM!!! 
 Scripture Reference. 
1 Samwel 30:8
2 Samwel 2:1
2 Samwel 5:19

Questions to be answered as you take your time to study this short lesson.
1. Can I really enquire of the Lord.
2. Is it necessary to enquire of the Lord.
3. What does enquire of the Lord imply?
And many more questions as the Spirit of God will be taking you through the lesson. 
Once again you are welcome.

2 Samwel 2:1 
And it came to pass after this, that David enquired of the LORD, saying, Shall I go up into any of the cities of Judah? And the LORD said unto him, Go up. And David said, Whither shall I go up? And he said, Unto Hebron.

Shall I go... Many are times that we move without permission but just because we think we can move. 
Sometimes we can really do it but sometimes the Lord has the best way to do it and its were we need to enquire. Basically we need to totally depend on Him. Enquiring is kind of submission onto the Lord. 
We don't willingly enquire unless we are able and ready to obey what He says. 
Enquiry is very important in times of great challenges.
As a servant of God, an ambassador of His Kingdom, a partaker of His Kingdom or a child of God, you really need a heart that asks from the Lord. 
CHOICES
When you've got choices. But you really can't figure out which one should start. 
You can't win in battles by depending only on your understanding. It is impossible to make it by your own counsel. Unless the Spirit of God is advising you in the inside about something that is going on. 

You can begin this by letting your thoughts align with the word of God and the will of God. Easily will your actions prove and glorify God.
Victory
You get assurance of victory through enquiry... 

The heart of Enquiry give God the glory.
Thank you may I end up here. Be blessed as you receive this message. 

Ref. 
1 Sam 30:8
And David enquired at the LORD, saying, Shall I pursue after this troop? shall I overtake them? And he answered him, Pursue: for thou shalt surely overtake them, and without fail recover all.
Judges 20:27
And the children of Israel enquired of the LORD, (for the ark of the covenant of God was there in those days,


#David Edwin 



Wednesday, December 16, 2020

Kumtumaini Bwana.

Kumtumaini Bwana. Hope in the Lord
Yeremia 10;23
Mithali 16:9 Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake.
A man's heart deviseth his way: but the LORD directeth his steps.

Mwana wa Mungu jifunze kumtegemea Mungu maana yeye ndiye kilakitu

Kumtumaini Mungu kunaweka nanga katika maisha yako, ni kuweka msingi bora wa maisha yako...
Yesu ni nanga imara.
Kumtumaini Mungu ni nanga imara.

GHARAMA YA USHINDI

  GHARAMA YA USHINDI 1. Utangulizi 2. Gharama ya ushindi 3. Kudumu kuwa mshindi Sehemu ya kwanza. Utangulizi   Kila jambo unalo ona limekwi...