Showing posts with label David Edwin. Show all posts
Showing posts with label David Edwin. Show all posts

Saturday, September 6, 2025

GHARAMA YA USHINDI

 GHARAMA YA USHINDI

1. Utangulizi

2. Gharama ya ushindi

3. Kudumu kuwa mshindi


Sehemu ya kwanza. Utangulizi 

Kila jambo unalo ona limekwisha fanyika, linafanyika sasa au imepangwa kufanyika baada ya wakati fulani, katika mpango wake Kuna kipengele cha gharama.

Gharama ya jambo inaweza kwa sehemu kubwa kuamua thamani ya Hilo jambo hilo ikishirikiana na matokeo yake. 

Tutajikita zaidi kuangalia gharama ya ushindi katika mambo yamuhusuyo mwanadamu hapa duniani. (Maisha) 

Kwa sababu maisha ni jambo pana lenye tafsiri nyingi nitajitahidi kueleza bila kutumia misamiati migumu na Kwa lugha inayoeleweka. Twende pamoja. . .

Gharama ni aidha muda, nguvu, fedha, mali, maumivu, ufahamu/ujuzi, aina ya maisha, aina ya kazi na mambo yanayofanana na hayo yanayofanyika ili kufanikisha jambo lililokusudiwa Kwa muda mfupi au muda mrefu. 

Mfano wapo watu waliolazimika kuishi maisha ya chini ili wahakikishe wanakamilisha ujenzi, wapo waliolazimika kuongeza ujuzi au kisomo ili wapate aina fulani ya kazi.

Zote hizo ni gharama za ushindi wa Yale waliyo yakusudia. 

Wakati unapanga kufanya jambo au kama hukupanga na umejikuta upo ndani ya jambo, jiulize swali la hili, "ni zipi gharama za jambo hili kufanikiwa?"

Unapozifahamu gharama ni rahisi kuishi kulingana na matakwa ya mafanikio ya jambo lako. 

Wakati mwingine kuzifahamu kunaweza kuhusishwa na woga au hofu juu ya jambo husika, lakini Bado ni muhimu sana kufahamu gharama za kushinda. 

Unapo ona biashara ya mtu inaenda vizuri ujue kabisa kuna gharama ya kusababisha iende hivyo. Unapo ona ndoa ya mtu inaenda vizuri ujue Kuna gharama! Unapo ona maisha ya mtu kidogo yanaenda sawa ujue kuna gharama. 

Kwa lugha nyingine rahisi ki tekinolojia, Kila mara tunachaji vifaa vyetu vya mawasiliano ili kuhakikisha tunaweza aidha kupatikana au kuwapata tunaowatafuta. 

Vivyohivyo tunaweka salio kwenye vifaa hivyo ili tuweze kuwa hewani. Maana yake tumeingia gharama ya kuhakikisha yaliokusudiwa yanafanikiwa. 

Zoezi

1. Andika mambo matatu unayojishughulisha nayo katika maisha yako.

2. Ainisha gharama ya mambo hayo. 


Sehemu ya pili. Gharama ya ushindi 

Kwa kiasi sasa tumeshatambua tunacho kumbushana. 

Zifuatazo ni gharama ambazo zinahusika katika kufanikisha ushindi wa mtu au watu katika jambo lililokusudiwa. 

1. Uhusiano na Mungu. 

Huu ni msingi mkuu wa ushindi. Msingi huu unaweza kujitosheleza kabisa kwa ajili ya ushindi. 

Mahusiano na Mungu yanapimwa kuanzia kiwango cha matumizi yako ya muda. 

 Uliongea na Mungu lini mara ya mwisho wewe peke yako, Kwa sababu yako mwenyewe, au kuhusu biashara yako, au kuhusu ndoa yako, kuhusu mradi wenu, taasisi au jamii yenu..? 

Umetenga muda kwa ajili ya mambo yako yote lakini je Mungu amepata nafasi katika muda wako wa siku? 

Sisemi kwamba Kila siku uende kukusanyika katika ibada, ila nasema kwamba Kila siku unaweza kuwa na muda mfupi wa kuzungumza na Mungu wako. 

Amebarikiwa mtu yule amtegemeaye Bwana, atakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya maji.. Mtu anayeboresha mahusiano yake na Mungu ameunganishwa na asili ya mafanikio yake moja kwa moja. Haishiwi, hafilisiki, harusi nyuma kwasababu ameunganishwa na vyanzo vya baraka, ameunganishwa na vyanzo vya ufahamu bora Kwa ajili ya mafanikio yake. ( Mimi ni Mungu nikufundishaye ili upate faida). Taasisi yenye mahusiano na Mungu kadhalika haiwezi kurudi nyuma. 

Kuweka mahusiano mazuri na Mungu ni sawa na kuweka mahusiano na mafanikio yako. 

Wengi hujiuliza nitaanzia wapi au mbona Nina mahusiano mazuri na Mungu. 

Kwa mtu binafsi unaweza kuanza na hii. 

     Kila asubuhi unapojiandaa tenga dakika Tano za kumweleza Mungu kuhusu ratiba yako ya siku husika kisha mwombe akutangulie. Inapofika mchana, angalia dakika tano mueleze kuhusu siku yako jinsi inavyoenda na kumshukuru. Dakika tano tu sio nyingi. Inapofika jioni unaporudi mahali unapojipunzisha, kabla ya mambo mengi, mda mfupi Tena dakika tano mshukuru Mungu kwa siku na tambua aliyokusaidia ukiweza kuandika mahali ni vizuri zaidi. Jikabidhi tena mbele zake kwa muda huo. 

Kwa taasisi kabla ya mambo kuanza, katikati ya siku na baada ya kumalizia siku ifanyike hivyo. Kinachojengeka hapa ni ule utamaduni wa mawasiliano na Mungu. Na ndani yake utamaduni wa ratiba na mpangilio wa siku. Baada ya hapo utamaduni wa kupata mtazamo wa wiki, mwezi hadi Mwaka kuhusu yale uliyokusudia.

Uhusiano wako na Mungu ujikite kumfahamu. Aliwapenda zaidi watu wa namna gani au anafurahishwa na watu gani. Ni kina nani anao wafanikisha.?

Utaona Mungu anawapenda wale wanaompenda, anatokea Kwa wale wanao mtafuta, anawafanikisha wale wanaojibidiisha huku wakintegemea, anawasamehe wale eanaosamehe wengine, anafanya kazi na wale wenye kupenda kumfahamu, anawaongezea baraka wale wenye ufahamu wa kuzimudu au wenye utayari wa kuongeza Maarifa ya kuzimudu baraka hizo. 

Hivyo Kila anayeboresha mahusiano yake na Mungu anaweza kuwa mshindi katika mambo yamuhusuyo. 

Zoezi
Andika mambo kumi uliyofanya siku ya Leo.
Katika mambo hayo, kuna lililojikita kuboresha uhusiano wako na Mungu moja kwa moja? 

2. Uhusiano na watu

Kwasababu huwezi kumpenda Mungu usiye mwona wakati jirani unayemwona unamchukia, na kwasababu Mungu huwatumia watu ili kufanikisha mtu basi ufahamu ukiwa na huduma yeyote unayoitoa kwa jamii au ukihutaji huduma yeyote utahitaji watu. 

Uhusiano wako na watu utakuongezea sifa njema au sifa mbaya.  

Ili uweze kuwa mshindi ni muhimu kujifunza tabia za watu na namna ya kuhusiana nao, kuzifahamu tamaduni zao, maisha yao na mambo wanayoyataka ili uweze kujua ni mpaka gani usivuke na ni wapi hadi wapi ufike bila kuathiri mahusiano Yako na Mungu

Husiana na watu sana kwa kila namna nzuri lakini hakikisha mahusiano yako na Mungu hayaharibiki. 

Sehemu ya tatu . Kudumu kuwa mshindi

Ni rahisi tu, kuendelea kufanya yake yaliyokugikisha katika ushindi ni njia Bora ya kutunza ushindi wako. Bila kusahau kuongeza ufahamu kila mara juu ya namna ya kuendelea kudumu hapo.

Mambo yanayosababisha ushindi kuondoka katika maisha ya mtu, taasisi,familia au jamii.

1. Majivuno. Hali ya kuona kwamba ni kwasababu ya nguvu na juhudi zako au zenu 

Maneno ya kejeli kwa walio chini au ambao hawajafikia hatua hiyo. 

2. Tamaa. Tamaa ya mali au tamaa ya mwili. Kuipa nafasi tamaa kunasababisha mahusiano yaako na Mungu yanaharibika na hivyo mahusiano yako na ushindi wako, huondoa heshima yako kwa jamii yako na hivyo kubandua kidogo kidogo mafanikio yako kama ukoma. 

3. Marafiki/ washauri wabaya. 

Ukikosa ushauri mzuri au watu uliowafungulia moyo wako wakiwa waovu basi jiandae kuelekea njia hiyo hiyo. 

Jitahidi kuepuka marafiki wasio faa kwa gharama zote. 

Usiifiche Imani yako wala usimfiche Mungu wako mana yeye ndiye chanzo cha mafanikio yako. 

Hayo na yanayofanana na hayo yakifanikiwa kuharibu mahusiano yako na Mungu basi ufahamu umepoteza ushindi wako tayari hata kama Bado unaonekana kushinda. 

Mungu akubariki kwa wakati wa kujifunza. 

@David Edwin +255 754 914 944

Tuesday, March 28, 2023

THE GOOD WINE 🍷

THE GOOD WINE  🍷
John 2:10
And saith unto him, Every man at the beginning doth set forth good wine; and when men have well drunk, then that which is worse: but thou hast kept the good wine until now.

Shalom brethren!
I wanna speak a little bit about
 "THE GOOD WINE" 
 As from our reference.. There's a norm that people are used to. There's a traditional practice of doing or handling things. 
Traditionally there are double standards. If not with economic aspect then age, if not age, then popularity, position/authority, gender, tribal, region/origin and any other phenomena that can be used to group people.

Have you ever walked to a parking with reservations? What about an event with seats reserved for so and so...
So let's go now..
1. At the beginning.•°••°•
 External appearance of something,. Before understanding the innermost characters of something/someone. 
Before getting into it
Before you start that ministry 
Before you start that behavior/lifestyle
Before you get into that crew of gamblers
Before you begin to pursue her/him
Before you start going for your dreams/purpose 
Every man at the beginning doth set good wine..


2. And when men have well drunk..° °•°•°•°
After you get what you thought you saw, or needed. After you've achieved getting her heart/his affection. 
After you've married her/him
After you've got into something you thought it was pleasant/ that would give you joy/peace/ pleasure 
When you've now come to a place of achievement
When you've now successfully managed your credits
When you've got all you wanted/prayed for.

3. Then that which is worse is brought°•°•°°••°•••
When the ups and downs arise a real character mist show up
When temptations rise some people astray from from the will of God.
Some forget or neglect the standards after achieving their goals. 
They don't offer the best service again.
No longer available in church service.
Not humble as in the beginning.. they've got what they wanted.
Not hardworking anymore
They are not ready to serve again, love again or cherish their spouses. They've arrived where they wanted to.
Now you're with the real person
With the original somebody
No more camouflages 
You can only see the true colors.
 
4. But thou hast kept the good wine until now. 🍷
What does keeping good wine until now mean? 

Maintaining the standards of..
Quality
Holiness 
Righteousness
Hard working
Love
Concern
Care
Humbleness
Wisdom
Humility
The outside you being the same as the inside you
Character etc...

Generally can we just conclude it as Taste/ Ever-tasty

Qn. How can this be achieved?
Here's a clear simple way to make it.
Jesus did a miracle He turned water into fine/good/standard wine.
What ever you need/you've been through in your life, just repent and pray this short powerful prayers with me. 
   Jesus, I believe that you are the son of God, and that you gave your life on the cross that I may have everlasting life. 
Please forgive all my sins and make me whole again.
In Jesus name I pray. Amen

Dear brethren. What you've done is now like filling  your water pots with water. Jesus is going to turn that water into fine-good wine. 

Be blessed as you live a life of testimonies in Jesus name. 
EVER-TASTY

GHARAMA YA USHINDI

  GHARAMA YA USHINDI 1. Utangulizi 2. Gharama ya ushindi 3. Kudumu kuwa mshindi Sehemu ya kwanza. Utangulizi   Kila jambo unalo ona limekwi...