Thursday, October 17, 2019

Siri ya kujazwa nguvu kila wakati. The secret of being filled with power all the time.

Bwana Yesu asifiwe!
Praise the be to Jesus!
I want we take a short time to the secrets of being filled with power ( holy spirit power) all the time.
Nataka tuchukue muda mfupi kuangalia siri za kujazwa nguvu ( nguvu za roho mtakatifu) kila wakati.

Tutazame maandiko...
Let's see the scriptures....

Marko 1:35
Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.

Mark 1:35
And in the morning, rising up a great while before day, he went out, and departed into a solitary place, and there prayed.

Tunamuona Yesu akiondoka alfajiri na mapema kujitenga mahali na kuomba.
-(Asubuhi na mapema = Inaonesha kitu cha kwanza kabisa na cha thamani)
-(Mahali pasipokuwa na watu= Inaonesha utulivu na kujitenga mbali na kila mawazo na fikra za tofauti zozote)
-(Kuomba=Inaonesha kumwitaji Mungu na kunyenyekea kwake)

We see Jesus departing in early morning to a solitary place and praying.
-(Early morning=Shows the first valuable thing)
-(Solitary place=Shows a quite place away from any disturbances and every disturbing thoughts)
-(Praying=Shows the humbled heart and one in need of God's assistance)

So before we take a leap to other secrets lets take a close look on to this one as a question..
Do you have time to refuel/refill and strengthen your spirit?
Yes you fasted last week but God has new things for you everyday!
  Take time to a solitary place severally and your connection with the Holy spirit will be strong his powers will be coming out from you every time.

Hivyo kabla ya kupiga hatua kuangaliasiri zingine, tuangalie hii moja kama kwa swali...
Je una muda wako wa kujiimarisha? Na kuimarisha mahusiano yako na Mungu?
Ndio ulifunga wiki Jana lakini kumbuka Mungu anamambo mapya kwa ajili yako kila siku.
Chukua hatua uwe na muda wa kujitenga Mara kwa Mara na muunganiko wako na roho mtakatifu yataimarika sana zaidi nguvu zake zitatoka ndani yako kila siku kila saa..

Other secrets
-The word of God
Siri zingine
-Neno la Mungu

Be blessed as you follow.....
Ubarikiwe unavyozidi kufuatilia....

Why publishing everything to everyone? Kwanini utangaze kila kitu kwa kila mtu?

Should I publish and blaze about everything that God has done for me?
Je ni lazima nitangaze na niseme kila kitu alichonitendea Mungu?
Praise be to the Lord Jesus Christ!! Bwana Yesu Kristo asifiwe!!

Tunaishi katika dunia yenye mapambano mengi na vita vilivyojificha sana. Ni muhimu sana kushudia yale mambo Mungu amekutendea, lakini sio sheria ushuhudie kila kitu. Kumbuka sio watu wote wanaokusikiliza wanayafurahia hayo hivyo sababu hii inatupa msingi wa kuwa na kiasi katika kushuhudia/ kuyasema yale ambayo Mungu ametutendea.
We live in a world with so much wars and hidden battles. Yes it is important to share and publish the things that God has done for us yet its not necessarily a law that you must share everything.
Remember that not everyone that listens to you are happy and comfortable about what you share and publish. Then this gives us a foundation of the measure what we should share and what we shouldn't.
What do you share with whom do you share and when do you share!
Look at the scriptures....
Tazama maandiko....

Marko 1:44.              
akamwambia, Angalia, usimwambie mtu neno lolote, ila enenda zako ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe alivyoamuru Musa kwa kutakasika kwako, iwe ushuhuda kwao.

Mark 1:44
And saith unto him, See thou say nothing to any man: but go thy way, shew thyself to the priest, and offer for thy cleansing those things which Moses commanded, for a testimony unto them.

Why speaking out everything?
Kwa nini utangaze kila kitu?
         Je, utapata hasara gani au madhara gani katika hayo uyasemayo?

        What are the effects of publishing or sharing what you shouldn't share?

Let's take a look at the scriptures again...
Tuangalie maandiko tena....

Marko 1:45

Lakini akatoka, akaanza kuhubiri maneno mengi, na kulitangaza lile neno, hata Yesu asiweze tena kuingia mjini kwa wazi; bali alikuwako nje mahali pasipokuwa na watu, wakamwendea kutoka kila mahali.

Mark 1:45

But he went out, and began to publish it much, and to blaze abroad the matter, insomuch that Jesus could no more openly enter into the city, but was without in desert places: and they came to him from every quarter.

-We see here that Jesus could no longer enter the city openly.
-Tunaona hapa Yesu hakuweza tena kuingia mjini kwa wazi.

Its your time to evaluate your self, how many opportunities have you blocked out yourself by publishing everything, every time to everyone?, how many enemies have you increased through sharing what you were not supposed to share?

Ni muda wako wakujitathmini sasa, Ni fursa ngapi umejizibia kwa kutangaza kila kitu, kila Mara kwa kila mtu?, ni maadui wangapi umeongeza kwa kushirikisha na kutangaza yale ambayo hukupaswa kutangaza?

Be blessed as you continue following the word of life.
Ubarikiwe kama unavyoendelea kufuatilia neno la uzima.

Wednesday, October 16, 2019

MBEGU NA MAFANIKIO

MBEGU NA MAFANIKIO
Bwana Yesu asifiwe..
        Karibu katika siku yetu ya EEMC.
                           EEMC
ishi kwa malengo, timiza malengo yako.
Mfano wa kwanza.
Machine ya ATM na kadi ya ATM,
Ili utoe hela au upate hela, inabidi uwe na; kadi, Uwezo wa kufikia mashine ya kutoa hela, neno la siri la akaunti husika na pesa kwenye hiyo akaunti.

Tukubaliane Kuwa kila malengo yanamchakato wa kuyatimiza, kama hujaweka mchakato wakuyatimiza inamaana bado hayajawa malengo.

Litambue, lielewe kusudi lako, na kusudi la kufanya chochote ufanyacho.

Purpose,. Kivipi utatimiza malengo?
Tambua majira yako,
Kila mwanadamu anamajira makubwa mawili,
1-Kupanda
2-Kuvuna
Majira haya yana vitu vifuatavyo.
•Kunakuwekeza
•Mbegu
•Kukua
•Akiba
Mbegu
Kila mbegu inamajira yake ya Kupandwa,mahali pa kupanda, na namna ya upandaji.

MAFANIKIO YANATEGEMEA UFAHAMU WAKO JUU YA MAJIRA YA MBEGU ULIYONAYO.

Mtu anayefanya mambo kinyume cha utaratibu ameshindwa kutambua kusudi.

Kuwekeza.
Kuwekeza kwa ajili yako, Take care of your body, kanuni ya kwanza ya uwekezaji ni kuwa na afya nzuri.
Kula vizuri, mwili wako ni sehemu ya kwanza ya uwekezaji.
Weka bajeti nzuri ya kila matumizi yako.
Akiba
Weka akiba kwa ajili ya wakati ujao, itakusaidia kwa ajili ya kesho.
Weka akiba ya kuwekeza kwa ajili ya kesho, ili uweze kufikia malengo ya maisha yako.
    
     Ishi kwa malengo timiza malengo yako.

Wednesday, August 14, 2019

Confidence and Courage "Ev. Bernard Selemani.

What is your confidence??

Courage or Strength -
Means the heart to go on,
The mindset to dare
The faith towards your belief
The power to hold on despite of the challenge

1 Sam 17:31
Confidence means belief in your ability. Trusting that you can make it despite of the situation.

David a young man who was spirit filled had a courage and was confident to face Goliath with a strong determination of victory because he understood who/where his strength were from...
  He gives some experience about several trials that came his way as a Father's shepherd and compares to the current trial and gets a great assurance of victory...
How does confidence come?
Confidence comes through...
1-Understanding who is within you. Acknowledge Your God !!!

2-Being righteous-doing what is right before God, this will give you favour before God moreover it will enhance your prayer/communication with God.
Living righteous life assures you of the power of God within you.
Sin draws away confidence.

Have you lost the courage,? Here is a second chance.
God is calling for your heart back to him again!
Running away from salvation won't help you get that courage and confidence back but either it will destruct you completely.

Change your mind, come back to the cross

Yes you have been abandoned, yes you have messed up a lot.!.
It is enough Get up again and God will rebuild your strength within seconds of your decision.

As a believer make sure that you do what God said and if in anyway you are weak keep in mind that any weakness you got is not a guarantee for you to miss attend any program or calling that God has placed on you.

Let your Courage and strength be restored in Jesus mighty name

    ............  AMEN ................

Thursday, August 1, 2019

MBEGU NA MAFANIKIO

MBEGU NA MAFANIKIO
Bwana Yesu asifiwe..
        Karibu katika siku yetu ya EEMC.
                           EEMC
ishi kwa malengo, timiza malengo yako.
Mfano wa kwanza.
Machine ya ATM na kadi ya ATM,
Ili utoe hela au upate hela, inabidi uwe na; kadi, Uwezo wa kufikia mashine ya kutoa hela, neno la siri la akaunti husika na pesa kwenye hiyo akaunti.

Tukubaliane Kuwa kila malengo yanamchakato wa kuyatimiza, kama hujaweka mchakato wakuyatimiza inamaana bado hayajawa malengo.

Litambue, lielewe kusudi lako, na kusudi la kufanya chochote ufanyacho.

Purpose,. Kivipi utatimiza malengo?
Tambua majira yako,
Kila mwanadamu anamajira makubwa mawili,
1-Kupanda
2-Kuvuna
Majira haya yana vitu vifuatavyo.
•Kunakuwekeza
•Mbegu
•Kukua
•Akiba
Mbegu
Kila mbegu inamajira yake ya Kupandwa,mahali pa kupanda, na namna ya upandaji.

MAFANIKIO YANATEGEMEA UFAHAMU WAKO JUU YA MAJIRA YA MBEGU ULIYONAYO.

Mtu anayefanya mambo kinyume cha utaratibu ameshindwa kutambua kusudi.

Kuwekeza.
Kuwekeza kwa ajili yako, Take care of your body, kanuni ya kwanza ya uwekezaji ni kuwa na afya nzuri.
Kula vizuri, mwili wako ni sehemu ya kwanza ya uwekezaji.
Weka bajeti nzuri ya kila matumizi yako.
Akiba
Weka akiba kwa ajili ya wakati ujao, itakusaidia kwa ajili ya kesho.
Weka akiba ya kuwekeza kwa ajili ya kesho, ili uweze kufikia malengo ya maisha yako.
    
     Ishi kwa malengo timiza malengo yako.

Monday, July 22, 2019

UAMINIFU

                         UAMINIFU.
BWANA YESU ASIFIWE!!
Na Mwl....
.....Karibu katika somo letu la uaminifu.....

Mwisho wa somo hili utaweza kujijibu maswali haya na mengine mengi.

Uaminifu ni nini?
Mimi ni mwaminifu?
Je ninahitaji kuwa mwaminifu?
Inawezekana nikakosa uaminifu?
Je nahitaji uaminifu katika mambo gani?

Tuanze kuangalia haya.
Soma Mathayo 25:14 ..
Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri.
And unto one he gave five talents, to another two, and to another one; to every man according to his several ability; and straightway took his journey.

Ni wapi/kivipi tunapaswa kuwa waaminifu?
(A) Kuwa waaminifu mbele za Mungu,
  1Korintho 1:9
  1Korintho 4: 1-2
   Torati 7:9
Mungu Mwenyewe ni mwaminifu na yeye ni chanzo cha uaminifu

(B) Kuwa waaminifu kwa watu wengine.
Mathayo 24:45-47 Kuna kuiniliwa baada ya uaminifu,
Kama wewe sio mwaminifu unaiabisha imani uliyonayo wewe. Lakini pia uaminifu unathaminisha wokovu ulionao.

(C) Kuwa mwaminifu katika vyote ulivyo navyo(Mali na mapato yako)
Haswaa! hapa imetupasa kuwa waaminifu katika suala moja msingi kabisa ZAKA na sadaka..
Usiwemwizi wa zaka uwe makini usikose mbingu..

MUNGU ANATUPIMA UAMINIFU KWA YAPI?

- Nafasi tunayompa katika maisha yetu ya kawaida, tunamtambua Mungu kama nani?

- Pesa umeipa nafasi ya ngapi... Siku za mwisho watu watapenda pesa kuliko kumpenda Mungu. Wapo wanaochukiana kisa pesa..

-Biashara au shughuli inayokuingizia mapato, wengi wamekamatwa hapa, maana unaweza ukategwa kwa wateja kuongezeka muda wa ibada.

-Nadhiri na maagano.
Muhubiri 5:4 Ukimwekea Mungu nadhiri usikawie kuiondoa, Mungu hawi radhi na wapumbavu.
  Ni afadhali usiweke kabisa kuliko kuiweka na kutoitimiza.
-Muda wako kwa Mungu, je unampa Mungu nafasi, kuanzia wewe binafsi?. Unashiriki maombi na taratibu zote za ibada?   !!!!!Jitathmini!!!!
Luka 16:10
Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.
He that is faithful in that which is least is faithful also in much: and he that is unjust in the least is unjust also in much.
Bila kuwa waaminifu haswa kwa mambo madogo kabisa hatuta mwona Mungu,
Nakazia tena sisi ni mabalozi wa Kristo hivyo imetupasa kuwa waaminifu sana mbele za Mungu na mbele za wanadamu.

Haijalishi ni tatizo ama uhitaji wa namna gani, sema kweli hata kama itakugharimu kwa sababu Uaminifu ni pamoja na ukweli.....
 
Usipende usingizi usije ukawa masikini, usingizi si hatar kwa maendeleo tu ya kiuchumi Bali hata kiroho, usiusikilize mwili ukaacha kuyatenda mapenzi ya Mungu..

Ukubwa au udogo wa jambo usikuchanganye!! Uaminifu ni katika mambo yote.

Mungu akubariki sana. Nakutakia wakati mwema.

Mwl. Faraja Komba

Monday, July 8, 2019

Hakuna mahusiano Bila Mawasiliano.

Na .Mwl Wetu..
Bwana Yesu asifiwe.
Developing Devotional relationship with God
Kuna aina saba za mahusiano
1: Wewe na Mungu
2: Wewe na mpenzi au mtu wa karibu sana mfano mke, mume au mchumba
3:Wewe na familia yako (mjomba n.k)
4: Familia hii na familia nyingine
5:Wewe  na Kanisa
6: Wewe na ufalme( wana wa Mungu ambao sio washirika wenzako katika kanisa moja)
7:Wewe na ulimwengu/dunia

Leo tutaangalia zaidi mahusiano kati yako na Mungu., haya yamebeba  msingi wa kila aina ya mahusiano unayopaswa kuwa nayo.

1. Uhusiano kati yako na Mungu  unaoneshwa na namna gani unamjua Mungu na kumpenda Mungu, Na kumjua Mungu nikulijua neno lake na kulitenda

Huwezi kusema unamahusiano na Mungu wakati huna mawasiliano naye.,Huenda mawasilano yenu yameingiliwa na jambo lingine..
   We have much time to pray but no time to listen from God.
Huwezi kuwasiliana na Mungu wakati wa uhitaji tu na ukasema unamahusiano mazuri na Mungu.
Ninyi mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu ombeni lolote ..
 
Listening .. Unauwezo wa kumsikiliza Mungu?
Je unasoma neno lake??
Develop a Conversation with God

Relational prayer, kuna wakati unapaswa kwenda Mbele za Mungu kuimarisha uhusiano wako na Mungu na sio kwenda mbele zake kila saa for your needs/probpems

Reference
Mwanzo 3:24
Dhambi inadhoofisha uhusiano wako na Mungu.
Yohana 17:3
Mwanzo 3:8
 
Watu wengi wa Leo wanamuda mwingi wa social network kuliko muda wao na Mungu, hawawezi au wamesahau kutafuta relationship na watu kuliko Mungu.
Vijana wanatafuta wenzi wao kwa juhudi kubwa kuliko kumtafuta Mungu na kuimarisha uhusiano wao na Mungu.
  Make a room for God in your heart
...
Mungu akubariki tutaendelea wakati mwingine kwa neema ya Kristo. Nakusihi sana imarisha uhusiano wako na Mungu.
*Spend more time with God!!

Barrier/kikwazo kikubwa katika mawasiliano yetu na Mungu ni dhambi na uovu, 
Tukaze mwendo watumishi wa Mungu..
.... To be continued......

Mahali Casfeta Tayomi Mwecau. Monday Service.

WATU WANGU WAJIBU WANGU. MY PEOPLE MY RESPONSIBILITY

 ✓ WATU WANGU WAJIBU WANGU ✓My people my responsibility *NI MUHIMU KUFAHAMU KWAMBA UNATAWAJIBIKA KWA WATU WAKO KATIKA MAMBO YOTE. YAANI YAKI...